-
-
by
Victor Abuso
Klabu ya soka ya Lweza FC, iliwaangusha mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka nchini Uganda Vipers FC kwa kuwafunga mabao 2 kwa 1 Jumanne jioni katika uwanja wa Wankulukuku jijini Kampala.
Mchuano huo ulitazamwa na maelfu ya mashabiki wa vlabu hivyo viwili nchini Uganda na kwingineko barani Afrika.
Kipindi cha kwanza, kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza hakuna klabu iliyokuwa imepata bao.
Hata hivyo, Lweza FC ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia mchezaji wake Juma Bagala katika dakika ya 69 lakini mshambuliaji wa Uganda Cranes Erisa Ssekisambu aliisawazishia Vipers katika dakika ya 85 ya mchuano huo.
Emmanuel Kalyowa alikuwa shujaa wa Lweza baada ya kuipatia timu yake bao la ushindi katika dakika za ziada za mchuano wao na kufanya matokeo kuwa mabao 2 kwa 1 hadi mwisho wa mchuano huo.
Lweza sasa ni ya 12 kwa alama 16 huku Vipers ikisalia katika nafasi ya pili kwa 28.
Ligi inaongozwa na KCCA kwa alama 29, katika michuano 15 iliyochezwa katika ligi hiyo hadi sasa.
Kikosi
Lweza F.C :
Charles Lukwago (G.K), Fred Okot, Nestroy Kizito, Mike Kabanda, Swaibu Mudde, Julius Mutyaba, Paddy Muhumuza, Fred Kalanzi (63′ Moses Ndawula), Juma Balinya (23′ Hassan Kikoyo), Emmanuel Kalyowa (80′ Geofrey Sserunkuma), Sula Bagala
Vipers SC :
Ismael Watenga (G.K), Nicolas Wadada (C), Aggrey Madoi, Halid Luwalira,Yusuf Mukisa, Deus Bukenya, Erisa Ssekisambu, Kezironi Kizito (51’Allan Kyambadde), Mike Mutyaba (61′ Mike Mutyaba), Ibrahim Saddam Juma (71′ Pius Wanji), Brian Nkuubi
Ligi hiyo itaendelea siku ya Ijumaa, URA itachuana na Maroons kuanzia saa 12 jioni.



CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup

CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 5 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...