-
-
by
Victor Abuso
Shirikisho la soka barani Afrika CAF, limewateua marefarii kutoka Swaziland kuchezesha mchuano wa mzunguko wa kwanza kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika kati ya mabingwa watetezi TP Mazembe kutoka DRC na St.George ya Ethiopia.
Mchuano huo utapigwa katika uwanja wa Bahir Dar siku ya Jumapili.
Marefarii hao wataongozwa na Mbongiseni Fakudze Elliot atakayesaidiwa na Petros Mbingo Mzikayifani na Sifiso Nxumalo.
Tarehe 20 mwezi huu, Mazembe watakuwa nyumbani katika uwanja wao wa Stade TP Mazembe kurudiana na wapinzani wao.
Klabu nyingine, ya DRC inayoshiriki katika michuano hii, AS Vita Club, itakuwa nyumbani katika uwanja wa Tata Rafael kumenyana na Clube Ferroviario ya Msumbiji.
Waamuzi wa mchuano huu ni kutoka Eritrea wakiogozwa na Amanuel Eyob Russom na kusaidiwa na Angesom Obgamariam pamoja na Suleiman Ali Salih.
Katika taji la Shirikisho, klabu ya CS Don Bosco itakuwa Misri kuchuana na Misr Makkassa siku ya Jumamosi, mchuano utakaosimamiwa na refarii kutoka Somalia Hassan Mohamed Hagi.
Wawakilishi wengine wa DRC katika michuano hii FC St Eloi Lupopo,watakuwa wenyeji wa El Ahly Shandy kutoka Sudan siku ya Jumapili katika uwanja wa Kibasa Maliba mjini Lubumbashi.



CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup

CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 5 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...