-
-
by
Victor Abuso
Timu ya Taifa ya soka ya Kenya Harambee Stars itamenyana na Taifa Stars ya Tanzania katika mchuano wa kimataifa wa kirafiki.
Mchuano huo utapigwa tarehe 29 mwezi Mei jijini Nairobi.
Kenya na Tanzania zitatumia mchuano huo kwa maandalizi ya mchuano wa kufuzu kucheza fainali ya mataifa bingwa barani Afrika, itakayofanyika nchini Gabon mwaka ujao.
Harambee Stars inajiandaa kucheza na Congo Brazaville tarehe 3 mwezi Juni huku Tanzania ikimenyana na Misri tarehe 4 pia mwezi huo.
Kenya ambayo haiwezi kufuzu katika michuano hiyo, ni ya mwisho katika kundi E, kundi ambalo linaongozwa na Guinea Bissau ikifuatwa na Congo kisha Zambia.
Tanzania nayo haina nafasi ya kufuzu kwa sababu Chad ilijiondoa na kundi hilo la G kwa sababu za kifedha, linasalia na Misri ambao kimahesabu wamefuzu na Nigeria tayari wameondolewa.
Rais wa Shirikisho la soka nchini Kenya Nick Mwendwa amesema, Harambee Stars inataka kuanza kucheza mechi za Kimataifa za kirafiki kwa mujibu wa kalenda ya FIFA.



CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup

CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 5 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...