Na Victor Abuso
Mataifa saba ya Afrika yatakayoshiriki katika michuano ya soka kuwania ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 23 itakayofanyika kati ya tarehe 28 mwezi Novemba hadi tarehe 12 mwezi Desemba nchini Senegal yameshafahamika rasmi
Mataifa hayo ni pamoja na wenyeji Senegal, Algeria, Misri, Zambia, Tunisia, Afrika Kusini, Nigeria na Mali.
Zambia, Tunisia na Mali zimefuzu katika michuano hii kwa mara ya kwanza.
Michuano ya mwisho ya kufuzu ilichezwa mwishoni mwa juma lililopita na washindi kupatikana.
Nigeria ilifuzu baada ya kuifunga Congo Brazaville mabao 2 kwa 1.
Algeria iliishinda Sierra Leone mabao 2 kwa 0, huku Mali ikiilaza Gabon mabao kwa 0.
Vijana wa Misri, waliwachabanga Uganda mabao 6 kwa 1, baada ya kushindwa mabao 4 kwa 0 jijini Cairo na nyumbani kulemewa kwa mabao 2 kwa 1.
Afrika Kusini nayo iliishinda Zimbabwe kwa jumla ya mabao 4 kwa 1, huku Tunisia wakiwalemea Morocco mabao 2 kwa 1.
Zambia baada ya kutoka sare ya kutofungana na Ivory Coast nyumbani na ugenini ilifuzu baada ya kupata ushindi wa penalti 4 kwa 3.
Michuano hiyo pia itatumiwa kutafuta timu tatu za kwanza kufuzu katika michezo ya msimu joto ya Olimpiki itakayofanyika nchini Brazil mwaka ujao.
CAF: Mataifa yatakayoshiriki fainali za Vijana yafahamika
CAF: Mataifa yatakayoshiriki fainali za Vijana yafahamika
More in
-
Nigeria Super Falcons break jinx and qualify for Paris 2024 Olympics
Nigeria Super Falcons have qualified for the 2024 Paris Olympic Games. Nigeria beat South...
-
Zambia Copper Queens qualify for 2024 Paris Olympics
The Zambia Women’s National Team, The Copper Queens have booked a place at the...
-
Cameroon sports Minister appoints Indomiable lions coach in Bizzare move
Cameroon Sports minister Narcisse Mouelle Kombi has appointed Belgian Marc Brys as the new...
-
Simba lose to Al Ahly at home in first leg Quarter-final
Tanzanian giants Simba SC suffered a devastating 1-0 defeat to record holders Al Ahly...