Connect with us

AFCON 2017: Ghana yailemea Msumbiji 3-1

AFCON 2017: Ghana yailemea Msumbiji 3-1

 

Black Stars ya Ghana ilindikisha matokeo mazuri siku ya Alhamisi baada ya kuifunga Msumbiji mabao 3 kwa 1 katika mchuano wa kundi H kufuzu kucheza fainali ya mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2017 nchini Gabon.

Mabao ya Ghana yalitiwa kimyani na Jordan Ayew, Frank Acheampong na John Boye huku bao la kufuta machozi la Msumbiji likifungwa na Apson Manjate.

Kwa matokeo hayo, Ghana inaongoza kundi lao kwa alama 9 baada ya kushinda mechi zake zote tatu ilizocheza hadi sasa.

Rwanda ambayo ni ya pili kwa alama 3, inajiandaa kumenyana na Mauritius ambayo pia ina alama tatu, siku ya Jumamosi katika uwanja wa Anjalay mjini Belle Vue.

Matokeo mengine ya siku ya Alhamisi, Madagascar ikiwa nyumbani ilitoka sare ya bao 1 kwa 1 na Jamhuri ya Afrika ya Kati, huku Comoros ikiwashangaza Bostwana kwa kuwafunga bao 1 kwa 0.

Djibouti nayo ikiwa nyumbani mjini Djibouti, ilifungwa na wageni wao Liberia bao 1 kwa 0.

Siku ya Ijumaa Machi 25 2016.

  • Swaziland vs Zimbabwe
  • Gabon vs Sierra Leon
  • Nigeria vs Egypt
  • Mauritania vs Gambia
  • Cote d’ivoire vs Sudan
  • Guinea vs Malawi
  • Tunisia vs Togo
  • Mali vs Equatorail Guinea
  • Algeria vs Ethiopia

Siku ya Jumamosi Machi 26 2016

  • Mauritius vs Rwanda

  • Seychelles vs Lesotho

  • Burundi vs Namibia

  • Congo DRC vs Angola

  • Cameroon vs South Africa

  • Cape Verde Islands vs Morocco

  • Burkina Faso vs Uganda

  • Senegal vs Niger

Siku ya Jumapili Machi 27 2016

  • Mozambique vs Ghana

  • Kenya vs Guinea Bissau

  • Bostwana vs Comoros

  • Congo vs Zambia

  • Benin vs South Sudan.

More in