-
-
by
Victor Abuso
Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA aliyesimamishwa kazi kwa tuhma za ufisadi, Sepp Batter amelazwa hospitali baada ya kusumbuliwa na msongo wa mawazo.
Msemaji wake Klaus Stoehlker amethibitisha kulazwa kwa Blatter na kuongeza kuwa anatarajiwa kuruhusiwa na kwenda nyumbani mapema juma lijalo.
Aidha, Stoehlker amesema Blatter mwenye umri wa miaka 79 ameendelea kusisitiza kupigania haki yake na kushtumu Kamati ya nidhamu ya FIFA kwa kumchukulia hatua ya kumsimamisha kazi kwa siku tisini hata bila ya kumsikiliza.
Binti wa Blatter Corinne amesema baba yake ameacha kukutana na watu hadi tarehe 15 mwezi Novemba ili kumpa nafasi ya kupata nafuu haraka.
Msemaji wa Blatter anasema masaibu yaliyompata katika siku za hivi karibuni yamemsababishia msongo huo wa mawazo huku akisisitiza kuwa hana kosa.
Sepp Blatter amekuwa akiongoza FIFA tangu mwaka 1998 na miezi kadhaa iliyopita alitangaza kuwa atajiuzulu na tayari ameitisha uchaguzi mpya kufanyika tarehe 26 mwezi Februari mwaka ujao wa 2016.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...