Na Victor Abuso, Klabu ya Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeondolewa nje ya michuano ya Shirikisho barani Afrika licha ya kupata ushindi wa mabao 3 kwa 2 dhidi ya Stade Malien katika mechi ya mwondoano mwishoni mwa juma lililopita. Mchuano huo ulichezwa katika uwanja wa Kimataifa wa Tata Raphael jijini Kinshasa. Stade Malien ilifuzu baada ya kupata ushindi katika mchuano wa mzunguko wa kwanza kwa kuwashinda AS Vita Club mabao 2 kwa 0 jijini Bamako. Vita club walistahili kupata ushindi wa mabao 3 bila ya kufungwa kuwa na uhakika wa kusonga mbele, lakini vijana wa kocha Florent Ibengé walishindwa kulifanikisha hilo. Msimu uliopita, AS Vita Club ilifika katika hatua ya fainali ya klabu bingwa barani Afrika. Katika matokeo mengine, Orlando Pirates ya Afrika Kusini imefuzu kwa jumla ya mabao 6 kwa 1 baada ya kuishinda Kaloum Star ya Guinea. Etoile du Sahel ya Tunisia licha ya kupoteza mchuano wa kwanza dhidi ya Raja Casablanca ya Morroco. CS Sfaxien ya Tunisia pia imefuzu baada ya kuishinda ASEC ya Cote Dvoire. Sanga Balende ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikaoondolewa na Zamalek ya Misri. Vlabu vingine vilivyofuzu katika hatua ya robo fainali ni pamoja na ES Tunis ya Tunisia, Al Ahly ya Misri na AC Leopard ya Congo Brazaville. Michuano ya robo fainali nyumbani ya ugenini zimeratibiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu, na Esperance de Tunis, Etoile du Sahel zote za Tunisia, Al-Ahly ya Misri na Stade Malien ya Mali zimejumuishwa katika kundi moja. Kundi lingine ni pamoja na Zamalek ya Misri, CS Sfaxien ya Tunisia, AC Leopards ya Congo na Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
CAF: AS Vita Club yaondolewa katika michuano ya Shirikisho
CAF: AS Vita Club yaondolewa katika michuano ya Shirikisho
More in
-
Nigeria Super Falcons break jinx and qualify for Paris 2024 Olympics
Nigeria Super Falcons have qualified for the 2024 Paris Olympic Games. Nigeria beat South...
-
Zambia Copper Queens qualify for 2024 Paris Olympics
The Zambia Women’s National Team, The Copper Queens have booked a place at the...
-
Cameroon sports Minister appoints Indomiable lions coach in Bizzare move
Cameroon Sports minister Narcisse Mouelle Kombi has appointed Belgian Marc Brys as the new...
-
Simba lose to Al Ahly at home in first leg Quarter-final
Tanzanian giants Simba SC suffered a devastating 1-0 defeat to record holders Al Ahly...