-
-
by
Victor Abuso
Klabu ya soka ya USM Alger kutoka Algeria siku ya Jumamosi inachuana na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika fainali ya kwanza ya klabu bingwa barani Afrika CAF mwaka 2015.
Mshindi atanyakua zawadi ya kitita cha Dola Milioni 1 nukta 5 na kufuzu katika fainali ya kombe la dunia baina ya vilabu itakayofanyika nchini Japan mwezi Desemba.
Fainali hii inatarajiwa kuwa ngumu na ya kusisimua na USM inafika katika hatua hiyo kwa mara ya kwanza, huku TP Mazembe wakiwa na uzoefu baada ya kushinda taji hilo mara nne mwaka 1967, 1968, 2009 na 2010.
Kikosi cha USM Algier kinaongozwa na kocha Miloud Hamdi, na wachezaji wake wengi ni wa nyumbani wakiwemo, Zinedine Ferhat na Mohamed Meftah bila kumsahau mshambuliaji wa Carolus Andriamanitsinoro.
Mazembe inayofunzwa na kocha Patrice Cateron kutoka Ufaransa inawashirikisha wachezaji wa nyumbani Ghana, Ivory Coast, Mali, Tanzania na Zambia.
Miongoni mwa wachezaji wa kuangaliwa katika kikosi cha TP Mazembe ni pampja na kipa maarufu Robert Kidiaba, Rainford Kalaba kutoka Zambia na Mbwana Samatta kutoka nchini Tanzania.
Hadi kufika katika hatua ya fainali, USM Algier ilishinda mechi zake zote sita katika hatua ya makundi na kufunga mabao 14.
TP Mazembe nayo ilifanya vizuri nyumbani na kufungwa mechi nyingi za ugenini huku akipata ushindi katika mchuano mmoja wa ugenini.
Fainali ya ili itachezwa tarehe 8 mwezi Novemba.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...