-
-
by
Victor Abuso
Mali itachuana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika fainali ya mchezo wa soka kuwania ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka nyumbani CHAN.
Mali ilifuzu siku ya Alhamisi baada ya kuifunga Ivory Coast katika mchuano wa nusu fainali jijini Kigali nchini Rwanda.
Yves Bissoouma ndiye mchezaji aliyeipa Mali bao la ushindi katika dakika ya 88 ya mchuano huo mgumu.
Baada ya mchuano huo, kocha wa Mali Djibril Drame amekiri kuwa timu ya DRC ni timu nzuri na anatambua mabingwa wa kwanza wa CHAN mwaka 2009 lakini, wachezaji wake hawaiogopi.
Aidha, Mali inajivunia idadi kubwa ya vijana chipukizi, kama Sekou Koita ,Abdoul Karim Dante, Mousa Sisoko na Mamadou Doumbia.
Nayo Leopard, kwa upande wake inajivunia wachezaji wengine wenye uzoefu wanaochezea klabu ya TP Mazembe, Vita Club na DC Motema Pembe wakiongozwa na nahodha Joël Kimwaki Mpela .
Maelfu ya mashabiki wa DRC pia wanatarajiwa kushuhudia mchuano huo kuishabikia Leopard.
Fainali itachezwa siku ya Jumapili katika uwanja wa Amahoro lakini itatanguliwa na mchuano kati ya Tembo wa Ivory Coast na Syli National ya Guinea kumtafuta mshindi wa tatu.



CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup

CAF Confederation Cup
Simba book final spot in CAF Confederation cup
Must See
-
AFRICA
/ 5 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 5 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...