-
-
by
Victor Abuso
Michuano ya soka ya CHAN kuwania ubingwa wa Afrika baina ya wachezaji wanaocheza soka nyumbani, intarajiwa kuanza Jumamosi ijayo tarehe 16 mwezi huu nchini Rwanda.
Mataifa 15 pamoja na Rwanda yatashiriki katika michuani hii inayitarajiwa kuwakusanya maelfu ya wapenzi wa soka katika nchi hiyo ya Afrika ya Kati.
Serikali ya Rwanda imetangaza kuwa hakutakuwa na malipo ya Visa kwa mashabiki wa mataifa yatakayoshiriki katika michuano hii watakaoamua kwenda nchini humo kuzishabikia timu zao.
Hii inamaana kuwa idadi kubwa ya mashabiki wanatarajiwa kushiriki katika michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini Rwanda.
Katibu katika Wizara ya Michezo Edward Kalisa, amesema,”Tumeondoa ada ya kupata Visa kwa wachezaji, mashabiki na wajumbe wa CAF kutoka mataifa yote yanayoshiriki katika michuano hii,”.
“Tunaamini kuwa hatua hii ya serikali itasababisha kuwepo kwa mashabiki wengi na hata kuongeza utalii nchini Rwanda na tayari tuna hoteli za kutosha kuwapokea wageni watakaokuja,” aliongeza.
Wiki hii kumekuwa na michuano ya kirafiki kwa maandalizi ya michuano hii, weyeji Rwanda wakicheza wiki hii na Cameroon walitoka sare ya bao 1 kwa 1.
Angola nao walipambana na Nigeria nchini Afrika Kusini na pia kutoka sare ya bao 1 kwa 1.
Siku ya Jumapili, kutakuwa na michuano kadhaa ya kirafiki kuendelea kujiandaa kwa michuano hii, Angola watacheza na Guinea, Uganda watamenyana na Gabon, huku Rwanda wakijipima nguvu na jirani zao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mataifa yatakayoshiriki ni pamoja na:Wenyeji Rwanda, Uganda, Ethiopia, Zimbabwe, Zambia, Angola, Gabon, Cameroon, DR Congo, Niger, Nigeria, Ivory Coast, Guinea, Mali, Tunisia na Morocco.
Mabingwa wa taji hili:-
DR Congo-2009 Michuano iliandaliwa nchini Cote D’voire
Tunisia-2011 Michuano iliandaliwa nchini Sudan
Libya-2014 Michuano iliandaliwa nchini Afrika Kusini



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...