-
-
by
Victor Abuso
Rais wa Shirikisho la soka nchini Zimbabwe ZIFA Cuthbert Dube amejiuzulu. Hatua hii imekuja wakati wajumbe wa soka nchini humo wakikutana siku ya Jumamosi katika Mkutano Mkuu wa soka na ajenda kubwa ilikuwa ni kupiga kura ya kukosa imani na kiongozi wao.
Dube amekuwa akiongoza soka nchini Zimbabwe kwa miaka mitano sasa na wakati wa uongozi wake, deni la Shirikisho hilo limeongezeka na kufikia Dola Milioni 6 na wachezaji wa timu za taifa wanaume na wanawake wamekuwa wakilalamikia malipo na safari zao kutatizika wanapokuwa na ziara nje ya nchi kutokana na uhaba wa fedha.
Wadau wa soka nchini humo wanajadiliana pia kuhusu uchaguzi wa tarehe 5 mwezi Desemba na wawakilishi wa Shirikisho la soka duniani FIFA na CAF wanashiriki.
Hata, hivyo Dube amesema kuwa ataendelea kusalia madarakani hadi viongozi wapya watakapochaguliwa.
Matatizo ya kifedha yameifanya FIFA kuizuia Zimbabwe kushiriki katika michuano ya kufuzu katika dimba la kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi baada ya kushindwa kumlipa kocha wake wa zamani wa timu ya taifa Mbrazil Valinhos Dola za Marekani 67,000.
Kocha wa zamani Tom Saintfiet pia amepeleka malalamishi yake kwa FIFA baada ya kutolipa fedha zake alipokuwa mkufunzi mwaka 2010. Saintfiet kwa sasa ni kocha wa Togo.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...