-
-
by
Victor Abuso

Klabu ya soka ya ES Tunis ya Tunisia na Raja Casablanca ya Morocco, zinamenyana kutafuta ubingwa wa taji la CAF Super Cup.
Huu ni mchuano ambao humkutanisha bingwa wa taji la klabu bingwa na Shirikisho barani Afrika baada ya kumalizika kwa msimu wa kutafuta ubingwa wa mataji hayo mawili.
Mechi hiyo itachezwa katika uwanja wa Thani Bin Jassim mjini Doha, kuanzia saa moja asubuhi saa za Afrika Mashariki.
Mechi hiyo ilikuwa imepangwa kuchezwa mjini Rades nchini Tunisia, mwezi Desemba mwaka 2018 lakini Shirikisho la soka barani Afrika CAF, lilitangaza kuwa mechi hiyo ingechezwa nchini Qatar.
Hii ni mara ya kwanza kwa mechi hii ya Super Cup, kuchezwa nje ya bara la Afrika na iwapo baada ya dakika 90 hakutakuwa na mshindi, hakutakuwa na muda wa ziada, mikwaju ya penalti itapigwa ili kumpata mshindi.
Fainali ya taji hili, inaashiria mabadiliko ya kalenda ya michuano ya klabu bingwa na Shirikisho ambayo itaanza mwezi Agosti na kumalizika mwezi Mei, kutoka mwezi February hadi Novemba.
Fainali ijayo ya taji hili, itachezwa mwezi Agosti, baada ya kumalizika kwa michuano ya mataifa bingwa barani Afrika itakayofanyika mwezi Juni hadi Julai mwaka huu.
Mabingwa watetezi wa taji hili ni Wydad Casablanca ya Morocco.
Al Ahly ya Misri imeshinda taji hili mara sita, huku TP Mazembe na Zamalek wakishinda mara tatu.
Etoile du Sahel na Enyimba ya Nigeria imeshinda mara mbili.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...