-
-
by
Victor Abuso
Mali na Nigeria zitachuana jumapili hii katika fainali ya kuwania kombe la dunia katika mchezo wa soka baina ya wachezaji wasiozidi miaka 17.
Michuano hiyo imekuwa ikifanyika nchini Chile tangu tarehe 17 mwezi uliopita wa Oktoba na bara la Afrika limeweka historia kwa kufika katika hatua ya fainali hatua ambayo imepongezwa na rais wa muda wa Shirikisho la soka duniani FIFA Isaa Hayatoue.
Mali ilitinga katika hatua hiyo baada ya kuifunga Ubelgiji mabao 3 kwa 1 huku mabingwa watetezi Nigeria wakiwafunga Mexico mabao 4 kwa 2 katika michuano ya nusu fainali iliyochezwa siku ya Alhamisi.
Mataifa 24 kutoka mabara 6 yamekuwa yakishiriki katika mashindano ya mwaka huu na mbali na Nigeria na Mali zinazocheza fainali, Guinea na Afrika Kusini pia kutoka barani Afrika yalishiriki.
Hadi sasa mfungaji bora ni Victor Osimhem kutoka Nigeria ambaye ametikisa nyavu mara 9.
Michuano ya kwanza baina ya vijana chipukizi wasiodizi miaka 17 ilianza mwaka 1985 nchini China.
Nigeria kutoka barani Afrika ndio nchi iliyofanikiwa zaidi katika michuano hii kwa kushinda mataji 4 ikifuatwa na Brazil iliyonyakua mataji 3.
Ghana na Mexico zimeshinda mara mbili na fainali ya mwaka 2017 itachezwa nchini India.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...