-
-
by
Victor Abuso
Shirikisho la soka duniani FIFA, limemruhusu mchezaji wa Kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joe Issama Mpeko kuichezea klabu ya TP Mazembe. Hatua hii inakuja miezi tisa baada ya kusajiliwa na klabu hiyo yenye makao yake mjini Lubumbashi akitokea klabu ya Kabuscorp nchini Angola. Mchezaji huyo ametia saini mkataba wa miaka mitano na Mazembe, na uongozi wa klabu hiyo umekuwa ukisuburi cheti kutoka FIFA kumruhusu mchezaji wake huyo mpya kuanza kucheza. Mpeko amesema amepokea kwa furaha kubwa habari hiyo na kuahidi kuwa atafanya bidii kuhakikisha kuwa anaisaidia klabu yake. Kocha wa Mazembe Mfaransa Hubert Velud, sasa ana uwezo wa kumchezesha mchezaji huyo katika michuano ya ligi kuu nchini humo lakini pia marudiano ya mchuano wa klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Casabalanca wiki ijayo mjini Lubumbashi. TP Mazembe ilifungwa ugenini mabao 2 kwa 0 na ina kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa inafunga zaidi ya mabao 3 ili kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele ili kutetea taji hili waliloshinda mwaka uliopita.
Related Topics



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...