-
-
by
Victor Abuso
Nahodha wa timu ya taifa ya soka ya Ghana Asamoah Gyan, ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya soka, wiki chache kuelekea fainali ya kuwania taji la Afrika nchini Misri.
Gyan amesema amefanya uamuzi huo baada ya kocha Kwesi Appiah kutomteua kuwa nahodha wa timu ya taifa wakati wa mashindano hayo makubwa barani Afrika yatakayofanyika mwezi Juni.
“Baada ya mashauriano na familia yangu na timu, iwapo uamuzi wa kocha ni kumpa unahodha mchezaji mwingine na ameniita katika kikosi chake, basi naomba nijiondoe,” amesema Gyan mwenye umri wa miaka 33.
Mchezaji hiyo anayechezea klabu ya Kayserispor nchini Uturuki, amesema amechana kabisa na timu ya taiga.
“Nastaafu kuichezea timu ya taifa, “ aliongeza.
Gyan alianza kuichezea timu ya taifa mwaka 2003 wakati akiwa na miaka 17 na katika mechi 106 alizoichezea, amefuga mabao 51.
Amewahi kuichezea Ghana katika kombe la dunia mwaka 2006, 2010 na 2014.
Kuelekea katika fainali ya AFCON, Ghana imepangwa katika kundi moja la F na Cameroon, Benin na Guinea-Bissau.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...