-
-
by
Victor Abuso

Bao la kusawazisha la Klabu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya, lilikataliwa katika mechi muhimu ya hatua ya makundi kuwania taji l;a Shirikisho barani Afrika dhidi ya timu ya NA Hussein Dey Jumapili usiku.
Bao hilo lilifungwa na beki kutoka nchini Uganda Shafik Batambuze katika dakika 59 baada ya mkwaju wa kona, na iwapo lingekubaliwa, mambo yangekuwa 1-1, lakini hilo halikubaliwa na mwamuzi kutoka Mali Boubou Traore.
Hatua hiyo, iliwakasirisha wachezaji na mashabiki wa Gor Mahia waliokuwa nchini Algier kushuhudia mechi hiyo.
Mechi hiyo ilikamilika kwa mabingwa wa soka nchini Kenya kupoteza kwa bao 1-0 na kuifanya Na Hussein Dey kuongoza kundi la D kwa alama saba.
Gor Mahia ni ya pili katika kundi hilo kwa alama 6, ikifuatwa na Zamalek ambayo ina alama tano baada ya kuishinda Petro de Luanda ya Angola bao 1-0 .
Al Hilal ya Sudan nayo imeendelea kupata matokeo mazuri baada ya kuishinda ZESCO UNITED ya Zambia kwa mabao 3-1 na inaongoza kundi la C kwa alama 7, ikifuatwa na Asante Kotoko ya Ghana ambayo nayo ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Nkana ya Zambia.
Etoile du Sahel ya Tunisia, nayo ikiwa ugenini iliishinda Enugu Rangers ya Nigeria mabao 2-0 huku Salitas ya Burkina Faso ikatoshana nguvu kwa kutofungana na CS Sfaxien.
Kundi A, RS Berkane ya Morocco inaendelea kuongoza kundi hilo kwa alama nane licha ya kutoka 0-0 dhidi ya ndugu zao Raja Casablanca lakini AS Otoho, ya Congo Brazville iliishinda Hassania Agadir ya Morocco bao 1-0.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...