Na Victor Abuso,
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka nchini Kenya Gor Mahia, wanahitaji kulinda ushindi wa mabao 3-1 waliopata dhidi ya klabu ya Lobi kutoka nchini Nigeria wiki iliyopita, ili kuandika historia ya kufuzu katika hatua ya makundi kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika.
Mechi hiyo ya marudiano itachezwa siku ya Jumamosi, mjini Enugu na Gor Mahia wanahitaji sare na kuzuia kufungwa katika mechi hiyo ili kufuzu, chini ya kocha wake mpya Hassan Oktay.
Hata hivyo, mabingwa hao mara 17 wa soka nchini mwao watakosa hudumu muhimu za kiungo wa kati Ernest Wendo ambaye katika anatumia adhabu ya kadi mbili za njano.
Gor Mahia, iliyoshinda kombe la Mandela mwaka mwaka 1987, haijawahi kufika katika hatua ya makundi tangu kuanzishwa kwa mfumo mpya wa kufuzu katika hatua hiyo.
Mechi nyingine muhimu Jumamosi Desembe 22 (Klabu bingwa):
ZESCO United vs TP Mazembe
Vipers vs CS Constantine
Jumapili
Simba vs Nkana.
Taji la Shirikisho Jumamosi Desembe 22:-
FS San Pedro vs DC Motemba Pembe
Asante Kotoko vs Kariobangi Sharks
Mukura Victory Sports vs Al-Hilal Al-Ubayyid



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...