-
-
by
Victor Abuso

Mabingwa watetezi wa taji la SportPesa, Gor Mahia ya Kenya, wameondolewa katika michuano hiyo, baada ya kufungwa na Mbao FC ya Tanzania kwa mabao 4-3 katika mechi ya mwondoano, kupitia mikwaju ya penalti.
Mchuano huo uliopigwa Jumatano mchana katika uwanja, wa Taifa jijini Dar es salaam nchini Tanzania, ulifika katika hatua hiyo baada ya kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Matumaini ya Gor Mahia kusonga mbele yalivunjika baada ya penalti ya nahodha Harun Shakava kuokolewa na kipa wa Mbao FC Metacha Mnata.
Wachezaji wa Gor Mahia waliofunga mabao ni pamoja na Francis Kahata, Jacques Tuyisenge na Boniface Omondi huku Said Hamis, Ngalema, Ibrahim Hashimu na David Mwasa wakiifungia Mbao FC.
Mbali na Gor Mahia, wawakilishi wengine wa Kenya AFC Leoaprds, nao wameondolewa katika michuano hiyo baada ya kufungwa na mabingwa wa soka nchini Tanzania Simba FC bao mabao 2-1.
Kuelekea katika michuano ya nusu fainali, klabu za Tanzania zilizofuzu ni pamoja ni Mbao, Simba huku Kenya ikiwa ikiwalishwa na Bandari na Kariobangi Sharks.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...