-
-
by
Victor Abuso
Kaimu rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Issa Hayatoue amesema anakabidhi baadhi ya madaraka ya kuongoza soka barani Afrika.
Uamuzi wa rais huyo wa FIFA ambaye pia ni rais wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF, unakuja kuelekea uchaguzi wa kumpata rais mpya wa FIFA mwezi ujao wa Februari.
Miongoni mwa mamlaka aliyoachia ni kuhusu kushughulikia uchaguzi ujao wa FIFA na mashirikisho mengine duniani, na sasa kazi hiyo itafanywa na manaibu wake wawili Suketu Patel ambaye ni Makamu wa kwanza wa rais na Almamy Kabele Camara makamu wa pili wa rais.
Hayatoue amechukua hatua hii ili kutoonekana kuwa na ushawishi wowote kuhusu uchaguzi wa FIFA.
Hayaoue alichukua nafasi ya urais wa FIFA baada ya Sepp Blatter kusimamishwa kazi mwezi Oktoba mwaka jana kwa tuhma za ufisadi.
Uongozi wa soka barani Afrika unatarajiwa kukutana tarehe 5 mwezi Februari kuamua ni mgombea yupi watamuunga mkono wakati wa uchaguzi wa rais mpya wa FIFA.
Mmoja wa wagombea hao Mwanamfalme wa Jordan Ali Bin Hussein amekuwa katika mataifa mbalimbali barani Afrika, kutafuta uungwaji mkono.
Wengine wanaowania ni pamoja na Sheikh Salman bin Ebrahim al Khalifa, Gianni Infantino, Tokyo Sexwale na Jerome Champagne.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...