-
-
by
Victor Abuso

Emerging Stars imejikwaa baada ya kufungwa na Sudan mabao 2-0 katika mechi ya kwanza iliyochezwa ugenini katika mchuano wa hatua ya pili, kufuzu kicheza fainali ya vijana wasiozidi miaka 23 barani Afrika, itakayofanyika mwezi Novemba nchini Misri.
Waleed Hamid ndiye aliyeifungia Sudan mabao yote mawili, bao la kwanza likitikisa nyavu ya Kenya katika dakika 33 huku bao la pili na la ushindi likifungwa kupitia mkwaju wa penalti katika dakika ya 75.
Kenya inahitaji kufunga mabao 3-0 itakapocheza na Sudan tarehe 26 mwezi Machi, katika uwanja wa Kimataifa wa Kasarani jijini Nairobi, ili kusonga mbele katika hatua ya tatu na ya mwisho ya kufuzu.
Matokeo mengine, DRC iliishinda Morocco mabao 2-0, Libya ikailemea Nigeria pia kwa mabao 2-0 huku Sudan Kusini na Tunisia wakishindwa kufungana.
Burundi ikicheza nyumbani dhidi ya Congo Brazaville, timu zote mbili zilimaliza mchehzo huo kwa kutofungana katika uwanja wa MwanaMfalme Loius Rwagasore jijini Bujumbura.
Mataifa nane, yatashiriki katika fainali hiyo, huku timu zitakazomaliza katika nafasi tatu bora, zitafuzu katika michezo ya Olimpiki itakayofanyika nchini Japan mwaka 2020.
Nigeria ndio mabingwa watetezi wa taji hili.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...