-
-
by
Victor Abuso

Kocha wa timu ya taifa ya soka ya Kenya Sebastien Migne amekitaja kikosi cha wachezaji 30 ili kuanza maandalizi ya michuano ya kuwania ubingwa wa mataifa ya Afrika, michuano itakayofanyika nchini Misri kuanzia mwezi Juni.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda nchini Ufaransa kuanza maandalizi ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika.
Migne raia wa Ufaransa, amemwacha nje beki David ‘Cheche’ Ochieng na mshambuliaji wa Zesco United nchini Zambia, Jesse Were.
Christopher Mbamba, anayechezea klabu ya Oskarshamns AIK nchini Sweden, ameitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha Harambee Stars.
Mshambuliaji Allan Wanga, ana kibarua cha kumridhisha kocha Migne kuwa katika kikosi cha mwisho cha wachezaji 23, pamoja na Michael Olunga, Masoud Juma na Ayub Timbe.
Harambee Stars ambayo imepangwa katika kundi moja na Algeria, Senegal na Tanzania, itakwenda kuanza maandalizi jijini Paris na kuondoka tarehe 18 kwenda nchini Misri, siku tano kabla ya michuano hiyo.
Kikosi cha awali:-
Makipa: Patrick Matasi (St. Georges, Ethiopia), Faruok Shikhalo (Bandari FC, Kenya), John Oyemba (Kariobangi Sharks, Kenya), Brian Bwire (Kariobangi Sharks).
Mabeki: Philemon Otieno (Gor Mahia-Kenya), Musa Mohammed (Nkana FC-Zambia), Joash Onyango (Gor Mahia-Kenya), Abud Omar (Sepsi Sfântu-Romania), David Owino (Zesco United-Zambia), Bernard Ochieng (Vihiga United-Kenya), Brian Mandela (Maritzburg United-Afrika Kusini), Erick Ouma (Vasalund IF-Sweden).
Viungo wa Kati: Victor Wanyama (Tottenham Hotspurs-England), Anthony Akumu (Zesco United-Zambia), Eric Johanna (IF Bromma-Sweden), Ismael Gonzales (UD Las Palmas-Spain), Francis Kahata (Gor Mahia-Kenya), Dennis Odhiambo (Sofapaka FC-Kenya), Johanna Omollo (Cercle Brugge-Belgium), Christopher Mbamba (Oskarshamns AIK-Sweden), Whyvonne Isuza (AFC Leopards, Kenya), Clifton Miheso (Ureno).
Washambuliaji: Paul Were (AFC Leopards-Kenya), Ayub Timbe (Beijing Renhe-China), Michael Olunga (Kashiwa Reysol-Japan), Allan Wanga (Kakamega Homeboyz-Kenya), John Avire (Sofapaka), Masud Juma (Libya), Ochieng Ovella (IF Vasalund, Sweden).



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...