-
-
by
Victor Abuso
Shirikisho la soka nchini Cameroon limemfuta kazi kocha wa timu ya taifa, Volke Finke.
Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya kikao cha Kamati kuu ya Shirikisho hilo siku ya Ijumaa kutokana na matokeo mabaya ya timu ya taifa.
Finke mwenye umri wa miaka 67 raia wa Ujerumani, amekuwa akiifunza Cameroon tangu mwaka 2013 na kikosi chake hakikuwa na matokeo mazuri wakati wa michuano ya kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil na fainali za taji la mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2015 nchini Equitorial Guinea.
Shirikisho la soka nchini humo Fecafoot limemteua Alexandre Belinga kuwa kocha wa muda na atasaidiana na Djonkep Bonaventure..
Kazi kubwa ya kocha huyo mpya ni kuiongoza Cameroon kufuzu katika fainali za kombe la dunia mwaka 2018 na mchuano wake wa kwanza utakuwa dhidi ya Niger tarehe 13 na 17 mwezi Novemba.
Cameroon ambao wakati mmoja walikuwa miamba wa soka barani Afrika, wameshindwa kurejea katika hali yao ya kawaida kama ilivyokuwa miaka mitano iliyopita.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...