-
-
by
Victor Abuso
Mshambuliaji Jacques Tuyisenge na beki Abouba Sibomana wanaoichezea klabu ya soka ya Gor Mahia nchini Kenya wamejumuishwa katika kikosi cha wachezaji 29 kuanza mazoezi siku ya Jumapili jijini Kigali.
Mchuano huo utakuwa maandalizi ya mchuano wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Senegal katika uwanja wa Amahoro mwishoni mwa juma lijalo.
Kocha Johnny Mckinstry amesema mchuano huo wa kirafiki ni muhimu kwa sababu atautumia kuwapima wachezaji wake.
Baada ya mchuano huo wa kirafiki, Rwanda itachuana na Msumbiji katika mchuano wa kufuzu wa mataifa bingwa barani Afrika mwaka ujao nchini Gabon.
Mchuano huo utapigwa mapema mwezi ujao.
KIKOSI KAMILI
Makipa:
Ndayishimiye Eric (Rayon Sports), Mazimpaka Andre (Mukura), Ndoli Jean Claude (APR), Nzarora Marcel (Police)
Mabeki:
Rusheshangoga Michel (APR), Omborenga Fitina (SC Kiyovu), Ndayishimiye Celestin (Mukura), Sibomana Abouba (Gor Mahia,Kenya), Imanishimwe Emmanuel (Rayon Sports), Nirisrike Salomon (STVV, Belgium), Bayisenge Emery (APR), Rwatubyaye Abdul (APR), Kayumba Soter (AS Kigali) and Manzi Thierry (Rayon Sports)
Voungo wa Kati:
Bizimana Djihad (APR), Nshimiyimana Imran (Police), Mugiraneza Jean Baptiste (Azam, Tanzania), Mukunzi Yannick (APR), Niyonzima Ali (Mukura), Habyarimana Innocent (Police), Sibomana Patrick (APR), Iranzi Jean Claude (APR), Hakizimana Muhadjiri (Mukura), Nshuti Dominique Savio (Rayon Sports), Habimana Yussufu (Mukura), Niyonzima Haruna (Young Africans)
Wshambuliaji:
Usengimana Danny (Police), Uzumakunda Elias (Le Mans, France), Tuyisenge Jacques (Gor Mahia, Kenya) and Sugira Ernest (AS Kigali).



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...