Connect with us

Michuano ya mwisho ya wanawake kufuzu fainali ya Afrika kuanza

Michuano ya mwisho ya wanawake kufuzu fainali ya Afrika kuanza

 

Michuano ya mzunguko wa mwisho mchezo wa soka kufuzu kucheza fainali ya mataifa bingwa barani Afrika kwa upande wa wanawake inachezwa kuanzia Jumatano hii.

Makala 12 ya mashindano haya yatafanyika nchini Cameroon kati ya tarehe 19 na tarehe 3 mwezi Desemba mwaka huu wakati wa michuano hiyo.

Mataifa nane ikiwemo wenyeji Cameroon yatashiriki katika michuano hiyo.

Leo, Jumatano Zimbabwe wanamenyana na Zambia, Tunisia na Ghana huku Mali wakiwa wenyeji wa Equitorial Guinea.

Siku ya Alhamisi,Misri watakuwa nyumbani kuchuana na Ivory Coast.

Warembo wa Algeria nao watakuwa nyumbani kupambana na wenzao kutoka Kenya siku ya Ijumaa, huku Senegal wakipepetana na Nigeria.

Boswatana na Afrika Kusini nao watachuana siku ya Jumamosi.

Ratiba ya michuano ya marudiano:-

Aprili 10 2016:-

  • Zambia vs Zimbabwe
  • Equitorial Guinea vs Mali

Aprili 11 2016:

  • Ivory Coast vs Misri

Aprili 12 2016:

  • Kenya vs Algeria
  • Ghana vs Tunisia
  • Nigeria vs Senegal
  • Afrika Kusini vs Botswana

Mshindi wa michuano hii itakayochezwa nyumbani na ugenini atafuzu katika fainali hizo.

 

 

More in