-
-
by
Victor Abuso
Misri imejiondoa kushiriki katika michuano ya soka katika mashindano ya Afrika yatakayofanyika mwezi ujao wa Septemba nchini Congo Brazaville.
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limethibitisha hatua hiyo ya Misri bila ya kutoa ufafanuzi wowote.
Hata hivyo, vyombo vya habari jijini Cairo vimekuwa vikiripoti kuwa kocha wa timu ya taifa Hossam El Badry anasema kikosi chake ni dhaifu.
Sheria za mashindano haya zinawaruhusu tu wachezaji wasiozidi miaka 23 kushiriki na miongoni mwa wachezaji shupavu wa Misri akiwemo kiungo wa kati Kahraba hatakuwepo wakati wa michuano hiyo.
Misri ilifuzu katika michuano hiyo baada ya kuishinda Kenya na Burundi katika hatua ya kufuzu.
Kuondoka kwa mabingwa mara mbili wa michuano hiyo kuna maana kuwa kundi lao linasalia na timu tatu Ghana, Nigeria na Senegal huku Burundi ikikataa kuziba pengo la Misri.
Michuano hiyo itafungua milango yake kati ya tarehe 6 hadi 18 mwezi Septemba na mataifa mengine yanayoshiriki ni pamoja na wenyeji Congo Brazzaville, Sudan, Zimbabwe na Burkina Faso.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...