-
-
by
Victor Abuso
Shirikisho la soka nchini Somalia SFF limetoa ratiba ya ligi kuu ya soka nchini humo mwaka 2016.
Ligi hiyo itaanza kupigwa siku ya Jumatatu juma lijalo na kutakuwa na vlabu 10 vitakavyoshiriki.
Dekedda FC itafungua ligi hiyo kwa mchuano kati ya Heegan FC hawa ni maafisa wa polisi ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo.
Kuwepo kwa wachezaji wa kulipwa kutoka nchi nyingine kumeifanya ligi kuu kuwa na ushindi mkubwa katika siku za hivi karibuni.
Msemaji wa SFF Shafi’i Mohyaddin Abokar amesema, “ Zaidi ya asilimia 95 ya raia wa Somalia wanapenda sana soka na tumeamua kuwa michuano itakuwa inachezwa kutoka siku ya Jumatatu hadi Ijumaa,”.
Viongozi wa soka nchini humo wanasema wanatarajiwa kuwa msimu huu mpya kutakuwa na ushindani mkubwa msimu huu.
Kuimarika kwa usalama nchini Somalia kumeleta matumaini ya kuendelea kwa soka nchini humo.
Wiki moja iliyopita kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, Shirika la taifa la Utangazaji SNTV lilionesha mchuano wa kuwania taji la Jenerali Da’ud.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...