-
-
by
Victor Abuso
Mwenyekiti wa klabu ya soka ya Gor Mahia nchini Kenya, Ambrose Rachier ametangaza kuwania urais wa Shirikisho la soka nchini humo FKF.
Rachier ambaye ni Wakili amesema baada ya mashauriano ya muda mrefu amefikia uamuzi wa kuwania wadhifa huo kwa lengo la kuinua mchezo wa soka katika taifa hilo la Afrika Mashariki.
Licha ya kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Gor Mahia, Rachier pia ni Mwenyekiti wa ligi kuu nchini humo KPL wadhifa alioupata baada ya klabu yake kuibuka mabingwa miaka mitatu iliyopita lakini pia ndio mabingwa wa mwaka huu.
Chini ya uongozi wa Rachier, Gor Mahia imekuwa ikifanikiwa katika michuano ya ligi kuu nchini humo kwa misimu mitatu sasa na anasema uzoefu wake utamsaidia kulete mabadiliko katika mchezo huo.
Wagombea wengine ni pamoja na rais wa sasa Sam Nyamweya, aliyekuwa Makamu wake Sam Shollei na Mwenyekiti wa klabu ya Kariobangi Sharks Nick Mwenda.
Uchaguzi huo utafanyika tarehe 13 mwezi Novemba ukitanguliwa na ule wa Matawi mbalimbali tarehe 29 mwezi Oktoba.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...