-
-
by
Victor Abuso
Rais wa Shirikisho la soka nchini Kenya FKF Sam Nyamweya amekamatwa na maafisa wa polisi jijini Nairobi kuhusiana na matatizo yaliyowakumbuka wachezaji wa timu ya taifa ya soka Harambee Stars kabla ya safari yao kwenda nchini Cape Verde siku ya Jumatatu usiku.
Wachezaji wa timu ya taifa walikwama katika uwanja wa ndege wa Wilson kwa saa nane baada ya mmiliki wa ndege waliyokuwa wamekodiwa na serikali kukataa ndege yake kuondoka kwa sababu nauli ya wachezaji haikuwa imelipwa kikamilifu.
Ilibidi serikali kuingilia kati kabla ya wachezaji hao kuondoka Jumatatu usiku na kusafiri kwa mwendo wa saa nane kabla ya mchuano wao dhidi ya Cape Verde kufuzu katika michuano ya kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Awali, wachezaji hao wakiwa kambini katika uwanja wa Kasarani waligoma kwenda katika uwanja wa ndege baada ya kulalamikia kutolipwa marupurupu yao kabla ya viongozi wa soka kutekeleza shinikizo zao.
Tukio hilo limezua hasira kwa wadau wa soka nchini Kenya na kutaka kukamatwa kwa Nyamweya kwa mkangayiko huo uliotokea.
Soka la Kenya limeendelea kukumbwa na tatizo la uongozi kwa kipindi cha muda mrefu na uchaguzi mpya wa viongozi wa soka unatarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...