Connect with us

Na Fadhili Omary Sizya,

Klabu ya Simba imesema inasubiri kupewa barua na Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania (TFF) inayoonyesha kweli wamepokwa pointi tatu za mchezo dhidi ya Kagera Sugar ili wakashitaki kwenye Mahakama ya usuluhishi ya FIFA (CAS) .

Simba ambayo ilipoteza mchezo huo mabao 2-1, ilikabidhiwa pointi tatu baada kamati ya usimamizi na uendeshwaji wa ligi (Kamati ya saa 72) kujiridhisha kuwa Kagera walimchezesha beki Mohamed Fakhi ambaye alikuwa na kadi tatu za njano kabla ya mchezo huo, pointi ambazo baadae zilirejeshwa kwa Kagera na kamati ya Katiba Sheria na Hadhi za Wachezaji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo hii, Rais wa klabu hiyo Evans Aveva amesema hawawezi kukubali kuona timu yao inaonewa tena na TFF, hivyo kwa kuanzia wanasubiri wapewe barua ya kuporwa pointi tatu hizo ili wapeleke malalamiko yao CAS.

Hata hivyo Simba inaongoza ligi kuu bara ikiwa na pointi 59 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 56.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

More in