-
-
by
Victor Abuso
Timu ya taifa ya soka ya Tanzania Taifa Stars itamenyana na The Fox Desert ya Algeria tarehe 14 mwezi wa Novemba katika mchuano wa nyumbani hatua ya pili kufuzu kwa fainali za kombe Dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi.
Mchuano huo utachezwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam kabla ya ule wa marudiano tarehe 17 mwezi huo wa Novemba jijini Algers.
Rais wa Tanzania akizungumza juma hili jijini Dar es salaam, ametoa wito kwa wachezaji wa Taifa Stars kujikakamua ili kuishinda Algeria nyumbani na ugenini ili kusonga mbele.
Kikwete amewaambia wachezaji wa Stars kuwa kazi kubwa ipo mbele yao.
Taifa Stars itapiga kambi nchini Afrika Kusini kwa siku 10 kuanzia tarehe 3 mwezi huu kabla ya kurejea jijini Dar es salaam kuikabili Algeria.
Taifa Stars ilifanikiwa kusonga mbele katika hatua ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga Malawi kwa jumla ya mabao 2-1, nyumbani ikishinda 2-0, na kufungwa 1–0 jijini Blantyre mwishoni mwa juma lililopita.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...