-
-
by
Victor Abuso
Timu ya taifa ya soka ya Burundi, Intamba Murugamba imeungana na Kenya, Tanzania na Ethiopia kutoka eneo la Afrika Mashariki na Kati kufuzu katika hatua ya pili ya kufuzu katika fainali ya michuano ya kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Burundi ilijihakikishia nafasi hiyo siku ya Jumanne, baada ya kuifunga Ushelisheli mabao 2 kwa 0 katika mchuano wa marudiano uliochezwa jana jijini Bujumbura.
Mchuano huo ulisimamishwa kwa muda kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jijini Bujumbura na viunga vyake lakini ukarejelewa tena baada mvua kumalizika na kufuzu kwa jumla ya mabao 3 kwa 0.
Burundi sasa inajiandaa kumenyana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mchuano wa mzunguko wa pili nyumbani na ugenini katikati ya mwezi wa Novemba.
Wawakilishi wengine wa eneo la Afrika Mashariki Sudan Kusini, ambao waliweka historia kwa kushiriki kwa mara ya kwanza katika michuano hii ya kufuzu, waliondolewa na Mauritania baada ya kufungwa kwa jumla ya mabao 5 kwa 1 licha ya kutoka sare ya moja kwa moja jijini Juba.
Somalia pia iliondolewa na Niger kwa kufungwa jumla ya mabao 6 kwa 0 nyumbani na ugenini.
Kenya itacheza na Cape Verde, huku Tanzania ikimenyana na Algeria katika mzunguko huo wa pili.
Uganda na Rwanda tayari zilikuwa zimefuzu katika hatua hii ya pili.
Mshindi wa mzunguko wa pili atafuzu katika hatua ya makundi.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...