-
-
by
Victor Abuso
Timu ya taifa ya soka ya Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia, Gabon , Morroco na Guinea zimefuzu katika hatua ya makundi kutafuta tiketi ya kufuzu katika kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Uganda Cranes walifuzu kwa jumla ya mabao 4 kwa 0 baada ya kuishinda Togo nyumbani na ugenini.
Mapema juma lililopita, Uganda walipata ushindi wa bao 1 kwa 0 mjini Lome, na baadaye kupata ushindi mkubwa wa mabao 3 kwa 0 nyumbani jijini Kampala huku mshambuliaji Farouk Maya akifunga mabao mawili .
Jamhuri ya Kideokrasia ya Congo maarufu kama Leopard nayo ilitoka sare ya mabao 2 kwa 2 na Burundi jijini Kinshasa baada ya kupata ushindi wa mabao 3 kwa 2 jijini Bujumbura.
Zambia waliishinda nyumbani na ugenini Sudan baada ya kuwafunga mabao 2 kwa 0 nyumbani na bao 1 kwa 0 ugenini.
Michuano hii inaendelea siku ya Jumanne.
Kenya watapambana na Cape Verde, Tanzania na Algeria huku Rwanda wakiwakaribisha Libya jijini Kigali.
Mataifa 20 yanatarajiwa kufuzu katika hatua ya makundi na mshindi katika kila kundi atafuzu katika michuano ya dunia.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...