-
-
by
Victor Abuso
Kocha wa timu ya taifa ya soka ya Uganda Milutin ‘Micho’ Sredojevic amekitaja kikosi cha wachezaji 27 kuanza maandalizi muhimu kumenyana na Togo kufuzu katika fainali za kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Mchuano huo utachezwa siku ya Alhamisi juma lijalo jijini Lome na kikosi hicho kinatarajiwa kuondoka jijini Kampala siku ya Jumatano kutumia ndege maalum iliyokodiwa na rais Yoweri Museveni.
Micho amesema ana imani na wachezaji aliowaita kambini.
“Nina imani kubwa na hawa wachezaji niliyowaita kwa sababu wamekuwa wakifanya vizuri katika vlabu wanavyochezea.Tunataka kuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchuano huo,” Micho ameimabia soka25east.com.
Mshambuliaji wa klabu ya Simba kutoka nchini Tanzania Hamis Kiiza ameitwa katika kikosi hicho pamoja na Ivan Bukenya anayecheza katika klabu ya Kaizer Chiefs nchini Afrika Kusini pamoja na Moses Oloya na Geofrey Baba Kizito.
Uganda na Togo watarudiana siku tatu baadaye jijini Kampala na mshindi atafuzu katika hatua ya makundi kutafuta tiketi ya kwenda Urusi mwaka 2018.
Kikosi kamili:
Makipa:
Denis Onyango, Salim Jamal, Robert Odongkara, James Alitho
Mabeki:
Dennis Iguma, Dennis Okot, Geofrey Walusimbi, Joseph Ochaya, Isaac Muleme, Shafiki Bakaki, Isaac Isinde, Ivan Bukenya, Murushid Jjuuko
Viungo wa Kati:
Tonny Mawejje, Aucho Khalid, Geofrey ‘Baba’ Kizito, Ivan Ntege, Yasser Mugerwa, Faruku Miya, William Luwaga Kizito, Muzamiru Mutyaba, Moses Oloya, Kezironi Kizito
Washambuliaji:
Geofrey Massa, Brian Umony, Hamis Kizza, Caesar Okhuti Ceaser



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...