-
-
by
Victor Abuso
Mabingwa wa soka nchini Misri Zamalek FC wamebadilisha uamuzi wao wa kujiondoa katika ligi kuu ya soka nchini humo.
Zamalek mwishoni mwa juma, walitangaza hatua hiyo baada ya kufungwa na klabu ya El-Gaish mabao 3 kwa 2 mchuano ambao wanasema mwamuzi wa mchezo huo aliwaonea.
Uongozi wa klabu hiyo ulikutana siku ya Jumatatu na kubadilisha uamuzi huo kutokana na adhabu ambayo ilikuwa inawasubiri ikiwa wangeendelea na uamuzi huo.
Ikiwa Zamalek ikiendelea na mpango wake, Shirikisho la soka nchini Misri lingeipiga marufuku ya mwaka mmoja klabu hiyo na kuishusha daraja.
Aidha, mabadiliko hayo yamefanyika baada ya mashabiki wa Zamalek kusema ni vema wasijiondoe kwa sababu ni mwaka jana tu waliposhinda taji la soka nchini humo baada ya muda mrefu.
Viongozi wa Zamalek wameamua kuliandikia Shirikisho la soka nchini humo kulalamikia namna mchuano dhidi ya El-Gaish ulivyochezeshwa na refarii Mahmoud Al Banna.
Al Banna alimpa beki wa Zamalek Ali Gabr kadi nyekundu katika dakika za mwanzo za mchezo huo na kuwapa wapinzani wake penalti mbili, hatua iliyowakasirisha viongozi wa Zamalek.



Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe

Africa Cup of Nations
Teams get tough opponents in AFCON 2025 Draws

Africa Cup of Nations
Tanzania,Uganda in tricky group with Nigeria and Tunisia

Africa Cup of Nations
Tough Afcon Group B as SouthAfrica paired with Egypt,Angola,Zimbabwe
Must See
-
AFRICA
/ 4 years agoSierra Leone FA President Isha Johansen endorses Patrice Motsepe for CAF President
Sierra Leone FA President who also doubles up as CAF Executive Council member Madam...
-
Football
/ 4 years agoIT JUST CAN NOT BE – AN AFRICA FULL OF MORONS?
By John De Mathews, There is an eerie silence around Africa, and it is...